Jumanne, 19 Desemba 2017
Njia 6 za kukabiliana na tatizo la kuziba kwa mirija ya uzazi
Kuziba kwa mirija ya mayai ya uzazi ni moja yaa sababu kubwa inayoweza kumpelekea mwanamke asipate ujauzito na hili ndilo chanzo kikuu cha wanawake wengi wanaoshindwa kupata ujauzito. Mirija hii ya uzazi ndimo ambamo mayai ya mwanamke hupita.
Mirija ikiziba ni kusema yai halitaweza kupita ili likutane na mbegu za mwanaume ili mimba iweze kutungwa nah ii ndiyo moja ya dalili kuu ya mirija ya uzazi kuziba. Mirija ya mayai hujulikana pia kwa kitaalamu kama ‘fallopian tubes’.
Sababu kuu ya kuziba kwa mirija ya uzazi ni maambukizi ya mara kwa mara ukeni ambayo hujipenyeza hadi ndani ya kizazi na kushambulia sehemu ya ndani ya kizazi na mirija. Maambukizi haya huambatana na muwasho, usaha ukeni, kutokwa na damu na uchafu wakati wa tendo la ndoa na kusikia maumivu chini ya kitovu.
Kuna wakati mirija haizibi bali hutokea mirija kuongezeka umbo sababu ya maji kujaa katika mirija ya maji na hivyo kupelekea mbegu za mwanaume kushindwa kupita kirahisi ili kukutana na yai. Halii hujulikana kitaalamu kama ‘hyrosalapinx’.
Dalili zitakazokuonyesha una tatizo la kuziba mirija ni pamoja na:
1. Maumivu chini ya kitovu ya mara kwa mara
2. Kusikia maumivu wakati wa tendo la ndoa
3. Kushindwa kupata ujauzito
4. Kutokwa na uchafu ukeni wenye harufu kali
Sababu ya mirija ya uzazi kuziba:
mbegu-za-maboga
>Magonjwa ya zinaa (PID)
>Upasuwaji uliopita wa sehemu ambazo si za kawaida kama katika tumbo na katika kizazi
>Mimba kutunga katika mirija ya uzazi (extopic pregnancy)
>Yai kutunga katika mdomo wa kizazi
>Utowaji mimba kila mara
>Mwili kuchafuka tu kwa ujumla
Nini unaweza kufanya ukigundulika mirija ya uzazi imeziba?
Kwanza fanya vipimo uonapo unatafuta ujauzito na hupati kwa kipindi cha walau mwaka mmoja. Kuna wengine wakiingia tu kwenye ndoa mara moja anahitaji kupata mtoto, hapana unaweza ksubiri hata mwaka ndipo ufanye vipimo. Vipimo vinapobaini ni kweli una tatizo la kuziba mirija ya uzazi unaweza kufanya yafuatayo kujinusuru na hali hiyo:
Njia 6 za kukabiliana na tatizo la kuziba kwa mirija ya uzazi
1. Acha vilevi vyote
2. Acha stress
3. Acha nyama nyekundu
4. Fanya mazoezi ya viungo kila siku
5. Kula sana matunda, mboga majani, mafuta ya zeituni, mafuta ya asili ya nazi
6. Kupata vitamin C kwa wingi tumia unga wa majani ya mlonge, kuongeza kinga yako ya mwili kwa ujumla tumia mbegu za maboga kila siku
Fuatilia mabadiliko haya kwa miezi miwili mpaka 6
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni
Comment yako ni muhimu sana