TIBA YA KANSA IPO?
Tiba ya kansa ipo Ni swali ambalo kila mtu anauliza na madaktari wameshindwa kutoa majibu ya uhakika hata mimi huwa najiuliza, maana nimeshuhudia watu wengi wakipata shida juu ya tatizo hili. Madactari watakwambia una kansa ya ini, utumbo, mapafu ama kizazi, lakini hawakwambii nini kimekufikisha kwenye tatizo husika, hivo tiba ya kisasa italenga moja kwa moja katika kutibu dalili ya kansa kama kuukata uvimbe kabla haujaenea sana, kuchoma uvimbe kwa kutumia mionzi, ama kutumia madawa makali katika kudhoofisha uvimbe wa saratani. Lakini je ulishawahi kujiuliza nini chanzo kikubwa cha tatzo hili ambalo linamaliza maisha ya wapendwa wetu kila siku.??
Tiba asili ama functional medicine inahimiza kwa mgonjwa na dactari kukaa pamoja na kuchunguza nini vyanzo vya ugonjwa. Hivo kwa kusuluhisha chnazo basi tayari unakuwa umetibu matokeo ambayo ndio dalili za ugonjwa. Hivo kwa upande wa tiba asili, mwili ni kama bustani ama shamba nzuri. Shamba hili lisipotunzwa vizuri basi magugu yataanza kuota na kumea.
Tiba ya mionzi na kukata sehemu ya mwili iliyoathiriwa na saratani siyo mbaya, lakini pia ni muhimu mgonjwa kufahamu njia sahihi za kujikinga ama kuzuia tatizo lisirudi tena.
KUTUNZA SHAMBA yaani mwili wako ni sheria ya kwanza katika kukinga mwili dhidi ya saratani
Tafiti zinaonesha kwamba kuna vitu vingi ambavyo tuviweka kwenye kundi la vihatarishi vinavyoweza kupelekea sararatani, mfano aina ya lishe, ukosefu wa mazoezi, msongo wa mawazo, sumu kwenye mazingira, vyote vinaweza kuchochea ukuaji wa saratani.
Hapa utagundua kwamba ili mmea ama mifumo yako ya mwili ikiwemo viungo kama moyo, figo nk viweze klufanya kazi vizuri basin i lazima pawepo na mazingira salama kwenye shamba ama mwili husika wa binadamu, vinginevyo hapatukuwa na usawa na ndipo magonjwa kama saratani yataanza kuibuka.
Sasa kumbe tunaweza kuimarisha kinga ya mwili na kuwa makini kwenye vyakula tunavyokula, tukabadilisha mtindo wa maisha ukawa siyo wa kutegemea vyakula vya viwandani.pia tunaweza kuimarisha uwezo wa mwili kundoa sumu, na kuweka uwiano katika vichocheo ama homoni, na pia kuhakikisha tunakuwa fikra chanya mda mwingi tukaondoa msongo wa mawazo na hivo kutengenea maingira ya hisia nzuri za mwili.
Saratani ama kansa ni matokeo ya kuwa na uwiano mbaya kwenye mifumo yetu ya mwili na hivo kupelekea kinga ya mwili kushindwa kupambana na seli hizi. Seli za saratani huanza zikiwa ndogo sana lakni miili yetu iliumbwa kupambana na magonjwa , hivo ni muhimu mwili kupaliliwa na kuwekewa virutubisho vya kuusadia uendelee kupambana na seli hizi za kansa kabla hazijaleta madhara.
Ifuatao ni hatua tano ambazo unaweza kuzitumia kuzuia saratani, ama kama tayari umeugua basi itakusaidia kuzuia kuenea kwa seli za saratani ndani ya mwili.
1.ACHANA NA SUKARI
Sukari husaidia kukua haraka kwa seli za saratani, na pi kukufanya kuwa na uzito mkubwa na kitambi., kisukari kinaathiri zaidi ya watu bilioni 1.7 duniani.
Punguza matumizi ya vyakula vya wanga na sukari, pia vilivyosindikwa na badala yake tuwe tunatumia zaidi vyakula vya mafuta, asili na visivyosindikwa.
2.EPUKA VYAKULA VINAVOLETA MZIO AMA ALEJI
Viambata kama glutein vinavyopatikana kwenye nafaka za ngano kwa kiasi kikubwa, vinapoingiau kwenye utumbo hupelekea kulegea kwa ukuta wa tumbo unaohusika na uvyonzaji wa chakula, hapa nataka uelewe kwamba katika mfumo wa chakula, sehemu panapofanyika uvyonzaji wa virutubisho hitwa small intestine ama utumbo mwembamba, hivo basi siyo kila kitu huruusiwa kupita hapa kwenda kwenye mfumo wa damu. Sasa kuta za utumbo ni kama chekecheke ambalo linazuia baadhi ya vitu hatari kupita kwenda kwenye damu, endapo chekecheke hili likiwa na matobo makubwa ndipo sumu na protin kubwa kama glution hupenya kuelekea kwenye damu. Na hapo mwili utaitikia kama adui kaingia hivo kupeleka askari wengi mahali husika kushambulia, sasa mashambulizi ya mara kwa mara hupelekea mahali husika kututumka na kuvimba.
3.IMARISHA MFUMO WAKO WA CHAKULA
Saratani nyingi hutokana na hitilafu kwenye mfumo wa chakula unaoteketezwa na lishe mbaya, hakikisha unapunguza kiasi cha protini kwenye mlo wako, badala yake tumia vyakula salama vya mafuta kama mayai ya kuku wa kienyeji, nyama kutoka kwa mnyama aliyekuzwa kwa kula majani na siyo nafaka, parachichi, na nazi. Tumia pia mafuta ya omega 3 kwa wingi kutoka kwenye vyanzo kama samaki ama unaweza kupata virutubisho hivi vya asili kutoka kwenye vyanzo sahihi.
4.MAZOEZI IWE NI KITU CHA LAZIMA
Kwa ujumla mazoezi hupunguza kasi ya utolewaji wa homoni ya insulin na hivyo kutengeneza mazingira hafifu ya uwepo wa sukari kwenye mwili, na hivo sukari ikiwepo kidogo hupunguza kasi ya kuenena kwa seli a kansa. Utafiti ulowahi kufanyika umeonesha kwamba mazoezi mfululizzo kwa miezi mitatu yanasaidia kuimarisha kinga ya mwili inayopambana na seli za kansa/saratani.
5.PATA USINGIZI WA KUTOSHA NA KUJIEPUSHA NA mazingira hatarishi yanayopelekea kuugua ugonjwa wa saratani, mazingira haya ni kama mionzi kutoka kwenye vifaambalimbali kama matumizi makubwa ya simu, tv, kemikali zinazotokana na dawa za kuua vimelea kwenye mimea na wanyama.
UTAFITI WA MIMEA UNASEMAJE KUHUSU TATIZO LA KANSA
Nchi kama china na Vietnam zinasifika kwa kuzalisha kwa wingi mimea mbalimbali ambayo imekuwa ikisaidia kutibu kansa stage ya kwanza na kusaidia kuzuia kusambaa kwa seli za kansa. Hivo gharama zake imekuwa kubwa sana ukizingatia mimea hii haipatikani hapa Africa. mimea hii ni kama
1. GINSENG, mmea huu husaidia
· kuongeza kiwango cha seli nyeupe za damu ambazo hupambana na seli a kansa, rejea hapo juu nlipoandika uhusiano wa kinga yako na kukua kwa seli za saratani.
· Pia mmea huu husaidia kharakisha uponaji wa vidonda na kutibu saratani ya awali.
2. CORDCEP SYNESIS husaidia
· Kuimarisha kinga ya mwili na hivo kuzuia mashambulizi ya mwili ya mara kwa mara
· Kupambana na seli za kansa
· Huimarisha ufanyaji kazi wa figo, ini na mapafu na
· Kuongeza nguvu kwa wale wanaopata ganzi mara kwa mara.
3. GARNODERMA, mmea huu husaidia
· kuimarisha kinga ya mwili na hivo kuzuia saratani.
· Kupunguza athari zinazotokana na tiba ya mionzi na madawa makali (radiotherapy na chemotherapy) nahivo kukupunguzia adha mablimbali kama kutapika, maumivu, kupungua kwa nywele, na ganzi ya mara kwa mara. Hivo unaweza kuendelea na dozi ya hospitali huku ukitumia dawa zetu pia.
· Kuongeza uwezo wa kinga ya mwili, na kusaidia wenye aleji na magonjwa ya mfumo wa hewa kama pumu na hivo kukuwezesha kurahisisha upumuaji.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni
Comment yako ni muhimu sana