Ijumaa, 12 Januari 2018

SAIKOLOJIA
Tabia za makuzi kwa watoto,Je unafahamu kuwa unapokuwa unaongea ukiwa na mtoto mchanga, anakuwa anakusikia na anakuelewa, au kuandika ujumbe kwenye simu au computer huku anatazama, anakuwa anasoma na kuelewa unachokiandika?

Inakuja kuthibitika atakapokuwa mkubwa, kwa kiasi fulani atafanana matendo kama ya kwako. Kwani alisoma ulichokuwa unaandika akiwa mtoto, akasoma, ufahamu wake ukajua kuwa huo ndio mfumo halisi wa maisha, au alikusikia ukiongea, akatambua kuwa huo ndio msingi wa kuishi kwenye maisha.

THIBITISHA. Mtoto akikua unamwita na kumtukania matukano ya ajabuajabu, ndivyo atakavyokuwa hadi ukubwani mwake, hali kadhalika ukiwa unamtamkia mema tangu utotoni kwa kudhamiria toka moyoni mwako, utamfanya mwanao kuwa ni mfano mwema, popote awapo, hata utu uzima wake. Tubadilishe vizazi vyetu kwa kufanya vitu vyema hasa mbele ya watoto.

SAIKOLOJIA

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Comment yako ni muhimu sana